
Najua miezi michache iliyopita kulifanyika uzinduzi wa lift ya kwanza kwenye gorofa jijini Mbeya (
BONGO TV) ambapo uzinduzi huu uliohudhuriwa na watu wanaozidi 200 kwa mujibu wa msemaji wa chama cha Waalimu, uliufanya mkoa huu uingie kwenye headlines za hata utani kwamba mtoto aliezaliwa siku ya uzinduzi huo amepewa jina la ‘
Mwakalifti‘
Habari mpya ya uzinduzi Mbeya sasa hivi ni kuzinduliwa kwa Mabasi ya Ndenjela Jet yanayofanya safari zake kwenye mikoa ya Mbeya, Dar na Rukwa kwa mujibu wa alphamsigwa.blongspot.com

Unaambiwa mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ndio alikua mgeni rasmi yani lakini
pia
vilevile uzinduzi huu ulihudhuriwa pia na mkuu wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi.

Mwanamke huyu aitwae Nusura ni mmoja wa madereva wa mabasi haya.

Huyu ni mmoja kati ya Makondakta wa mabasi haya.

Watu wakifatilia uzinduzi…

Burudani ikitolewa na msanii ajulikanae kama ‘Awilo’
Kama una chochote cha kuandika kuhusu hii tafadhali usisite kuacha comment yako hapa chini mtu wangu…
No comments:
Post a Comment