Friday, January 30, 2015



 
Unajua kuna nchi zinapiga marufuku watoto kupewa baadhi ya majina? Yako hapa…
sad-kid
Huku kwetu tuna utaratibu wa kuwapa watoto wetu majina tunayopenda, yapo majina ya watu maarufu kama viongozi, wanasoka, waigizaji na wengineo.
Kuna hizi nchi ambacho wao wamepiga marufuku baadhi ya majina kupewa watoto, list ni hii hapa.
New Zealand: Msajili wa Vizazi, Vifo na Ndoa nchi hii ameagiza baadhi ya majina kupigwa marufuku ikiwemo majina haya; Majesty, Queen Victoria, Lucifer na jina la Mafia No Fear.
VenezuelaWao wamezuia matumizi ya jina la Superman kwa kuwa ni gumu kulitamka.
Denmark: Wametoa list ya majina rasmi ambayo yako zaidi ya 7,000 mtoto akizaliwa anachaguliwa jina kati ya majina hayo, moja ya majina yaliyozuiwa huku ni jina la Monkey.
Brazil: Jina lililozuiwa huku ni jina la Saddam Hussein.
Mexico: Wamepiga marufuku mtoto kupewa majina ya Scrotum, Terminator, Burger King, Hitler na Virgin.
Uturuki: Mahakama imezuia mtoto kupewa jina la Osama Bin Laden
Portugal: Wao wamezuia jina la Tom.
Mfano hii ingekuja Bongo, majina gani ungependa yazuiwe wasipewe watoto wetu?
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta Facebook

 

Next post link


Matangazo tofauti




  BIBI ANAYEDHANIWA KUWA MCHAWI AKUTWA AKIWA UCHI HUKO MAGEUZI MJINI SHINYANGA.

Hapa ni katika mtaa wa Mageuzi kata ya Ndembezi mjini Shinyanga pichani ni wakazi wa Ndembezi wakishuhudia tukio hilo la aina yake lilovuta hisia za watu wengi jana huku wengine wakidai kuwa bibi huyo ni mchawi kutokana na kiburi alichokuwa nacho huku akidiriki kupiga watu na kwamba mikono yake inaonekana imekatwa panga na imekomaa sana ambapo wataalamu wa mambo walisema huenda bibi huyo huwa anajigeuza Fisi na kutembelea mikono.



Bibi(aliyeko pichani) ambaye hajulikani jina wala anakotoka na ndiyo huyo amezua kizaa zaa baada ya kukutwa nje ya nyumba ya mkazi wa mtaa huo aitwaye Suzana Mwandu akiwa uchi wa mnyama hajitambui huku akitembea kwa kutumia makalio yake.Baada ya kukutwa akiwa uchi wasamaria wema waliamua kumvalisha nguo kusitiri mwili ingawa bibi huyo alijaribu kuzivua lakini baadaye kutulia na kuanza kuzungumza maneno yasiyoeleweka.

Mwonekano wa mikono ya bibi huyo iliyoonekana kama imekatwa kwa mapanga na imekomaa kwa nyuma.


Blog hii iliyofika eneo la tukio haraka iwezekanavyo kama kawaida yake imeambiwa kuwa bibi huyo ambaye hakujulikana jina wala makazi yake awali alikuwa haongei na aliposemeshwa ndipo akaanza kuongea kwa lugha ya Kisukuma maneno yasiyoeleweka huku akisikika akisema wenzake wamemuacha alikuwa anaenda kwenye sherehe.



Hatimaye bibi akaweza kusimama na kuanza kufanya vituko vya kila aina.
Bibi akaamua kukaa na kuanza kutoa pesa alizokuwa amezifunga kiunoni kwa kwenye mfuko wa rambo laini uliokuwa umefungwa kitaalam

Bibi akiangalia pesa zake

Zilikuwa ni shilingi za hamsini hamsini,mia moja ,mia mbili,mia tano na elfu akaziweka kwenye kibakuli kilichokuwa eneo la tukio.

Kushoto ni mjumbe wa serikali ya mtaa wa Mageuzi Waziri Musa(CHADEMA) akisaidiana na wananchi wa eneo hilo kumwondoa bibi huyo kwenye nyumba ya mkazi wa eneo hilo.

Bibi akawekwa chini ya mti,hata hivyo akaendelea kufanya vituko na kuamua kulala juu ya mawe,angalia hapa chini.




Bibi akiwa amelala juu ya mawe kabla askari polisi hawajafika eneo la tukio leo mchana japokuwa bibi huyo amekutwa nyumbani kwa mtu saa moja asubuhi.

Askari polisi wakimwangalia bibi huyo.

Askari polisi wakitoa maelekezo kwa wananchi wa mtaa huo ambapo walisema serikali haiamini ushirikina hivyo kuwataka wananchi waondoke eneo la tukio na kumwacha bibi aendelee na safari yake kwani tayari alikuwa amepata nguvu na kuanza kutembea kwa miguu badala ya makalio kama mwanzo.
Askari polisi akiwa amembeba bibi huyo kumtoa kwenye mawe,na katika hali ya kushangaza bibi huyo alimng'ang'ania askari huyo.Mpaka malundeq blog inaondoka eneo la tukio saa 14:10pm wakazi wa Mageuzi walikuwa wameanza kutawanyika huku bibi huyo akiondoka katika mtaa huo-
 
 
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
 

Wednesday, January 28, 2015

Manny Pacquaio na Floyd Mayweather uso kwa uso Marekani.

big 6

Mabondia wawili nyota Floyd Mayweather na Manny Pacquiao hapo jana walikutana uso kwa uso ikiwa ni mara ya kwanza kukutana katika kipindi hiki ambacho pambano lao limekuwa likitajwa sana .
Mabondia hao walikutana kwenye uwanja wa American Airlines Arena ambako walikuwa wakitazama mchezo wa ligi ya mpira wa kikapu ya NBA kati ya Miami Heat na Milwaukee Bucks .
Pacquaio alihudhuria mchezo huo akiwa mgeni wa kocha wa Miami Heat Erik Spoelstra na Floyd kwa upande wake amezoeleka kama shabiki mkubwa wa Miami na amekuwa akihudhuria michezo mingi ya timu hiyo .
Mayweather na Pacman wakionekana pamoja kwenye mchezo wa NBA nchini Marekani .
Mayweather na Pacman wakionekana pamoja kwenye mchezo wa NBA nchini Marekani .
Mabondia hao walionekana wakizungumza kwa kifupi kabla ya kupeana mkono na kuagana huku kila mmoja akienda kivyake .
Hivi karibuni mashabiki wa masumbwi wamekuwa wakizungumza kuhusu pambano la mabondia hao wawili na kumekuwa na mazungumzo ambayo yanaendelea japo hayajaweza kufikia hatua yoyote nzuri .
Hapa walionekana kama wanabadilishana namba za simu .
Hapa walionekana kama wanabadilishana namba za simu .

Hapa walipeana mikono na kuagana
Hapa walipeana mikono na kuagana

big fight

Tuesday, January 27, 2015

HALI inazidi kuwa mbaya kwa mastaa wawili wa muziki wa Bongo Fleva wanaogombea unyota kimuziki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Saleh Kiba, safari hii yameibuka mapya kwa kila msanii kuogopa kumshika mkono mwenzake kutokana na imani za kishirikina.

Mashabiki wa Mbongofleva Ali kiba waliionyesha kumkubali zaidi kuliko, 'Daimond Platnumz' katika viwanja vya Leaders Club.

TUJIUNGE LEADERS 
Matukio hayo ya kusisimua yaliwatia hofu kubwa mashabiki na wadau wa muziki Bongo muda mfupi kabla ya nyota hao kukaribishwa stejini kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita.

HIRIZI ZAKUTWA UWANJANI
Kwa mujibu wa wanahabari wetu, katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni, kulikutwa hirizi zilizozagaa, zilizodaiwa kudondoshwa  na vijana waliokamatwa wakiwa wamevalia sare zenye majina ya mastaa hao wawili.


Thursday, January 22, 2015



Monday, December 15, 2014

HII SASA NI KUFURU!!! P-SQUARE WAWEKA SOFA {SAMANI} ZA DHAHABU NDANI YA NYUMBA YAO MPYA....


We Talking Money You Talking Nonsense’ huenda ikawa kauli nzuri kuelezea hiki walichokifanya P-Square kwa sasa.

Hakuna ubishi kuwa, kwa hiki walichokifanya sasa, na kama macho yetu hayatudanganyi kwa hiki yanayokiona, mapacha hawa wamefanya kufuru. Kama hii inayoonekana ni dhahabu kweli, basi P-Square, hela wanayo.
4eb1c8da43d911e3bc6522000ae91414_8

3799cde443d611e3be7422000a9e0172_8
Peter ameshare picha hizi nne ambazo wiki hii zitakuwa gumzo barani Afrika ambapo kwenye picha moja inayomuonesha pacha mwezie Paul akiwa amesimama kwenye sebule mpya inayoaminika kuwa ya nyumba yao mpya, ameandika ‘Goldenworld #blessed.’
8300d71043da11e399e522000a9e28c4_8
Kwenye picha nyingine, wanaoonekana wakiwa pamoja kwenye sebule hiyo iliyotawaliwa na kile kinachoonekana kama dhahabu zilizozunguka sofa za kuvutia na Peter ameandika: #2kings…… Work hard,play harder.’
7493d06843dc11e3a21b22000ae913ab_8
Picha nyingine inamuonesha Peter akiwa peke yake kwenye meza ya chakula, kubwa, iliyojaa vyombo vya thamani vya kuvutia na ameandika: A king in my own world…. #Blessed.”

Wednesday, January 21, 2015

Wolper Asikitika Jina Lake Kutumiwa na Coca Cola Bila Hata Kushirikishwa Wala Kulipwa!!!

Wolper Asikitika Jina Lake Kutumiwa na Coca Cola Bila Hata Kushirikishwa Wala Kulipwa!!!
    Kupitia ukurasa wake wa  kwenye mtandao wa INSTAGARM,  Wolper alifunguka;
    “Habari Followers pamoja na wa Tanzania wote ambao naamini huwa mnaingia katika page yangu ya insta.Nimepokea zawadi hii ya Coca cola kwa siku 6 .
    Na sio kwamba sikutaka kupiga picha kama wenzangu au ku post kama wenzangu,  nilikuwa natafakari kweli kampuni kubwa ya kitaifa na kimataifa inaweza kutumia gharama kubwa kuandika majina yetu bila kuchukuwa hata nafasi na heshima kubwa tuliyonayo kutushirikisha tu katika makubaliano ya kuandika majina yetu katika makopo yao.
    Maana naamini mafan's wa Wolper wangeweza kushare na Coca cola kutokana Jina Langu kuwa label katika makopo yao.
    Sasa Naamini tuna wanaharakati,wabunge,wanaSheria pamoja na serikali ambao huwa wanafwatilia wale wauza CD wa kariakoo basi Naomba Juhudi hizi mzihamishie huku katika kampuni hii kubwa ya kimataifa Coca cola ili kutetea haki za wasanii na sio kudhalilishwa kwa kiasi hiki jamani.
    Sijui kama wasanii wenzangu walilipwa siwezi kuwasemea lakini haya ni mawazo yangu binafsi”. Wolper aliishia hapo.

    Tuesday, January 20, 2015

    Tumesikia upande wa Irina – sasa Ronaldo azungumzia kuachana na demu wake



    Cristiano-Ronaldo-and-Irina-ShaykKwa muda wa takribani wiki mbili kumekuwepo na habari juu ya kuvunjika kwa mahusiano ya mwanasoka bora wa dunia Cristiano Ronaldo na mrembo/mwanamitindo Irina Shayk.
    Mapema wiki iliyopita msemaji rasmi wa Irina Shayk alithibitisha kwamba mrembo huyo wa kirusi ameachana na Ronaldo ambaye alikuwa na mahusiano nae ya muda wa miaka 5, hata hivyo tetesi juu ya chanzo cha kuvunjika kwa uhusiano huyo zikaendelea huku mama mzazi wa Cristiano Ronaldo akitajwa kuhusika.
    Mama mzazi wa Ronaldo, Dolares ametajwa kumkataa Irina kwa sababu haoni kama mwanamke huyo atafaa kuwa mzazi mwema kwa mtoto mdogo wa Ronaldo aitwaye Cristiano JR.
    Hata hivyo baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimaye Cristiano Ronaldo ameibuka na yeye amethibitishwa kwamba ameachana na Irina huku akiomba sasa jamii imuache na maisha yake binafsi.
    Katika taarifa aliyotoa leo kwa vyombo vya habari, Ronaldo alisema: “Ni kweli uhusiano wangu wa miaka mitano na Irina umefikia tamati. Kuachana ni uamuzi ambao tuliufikia wote wawili na kitu ambacho tunaamini ni sahihi kabisa kukifanya kwa sasa.
    “Natoa taarifa hii ili kumaliza maneno maneno juu ya maisha yangu binafsi,” – alimaliza Cristiano Ronaldo.

    Haya ndio ya H Baba kwa mashabiki wa mastaa wa muziki Tz, Ali Kiba na Diamond Platnumz…



    instagram-signMuimbaji Hamis Baba aka H Baba ambaye muda si mrefu na mkewe wanatarajia kupata mtoto wa pili kwenye familia yao, leo ameamua kuandika kwenye ukurasa wake Instagram kuhusu nini ambacho anakiona kwenye muziki wa mastaa wawili, Diamond Platnumz na Ali Kiba.
    Ujumbe huo unasomeka hivi ;Mie nawakubali wote kila mmoja ana ladha yake kwenye muziki wa #bongoflava chamsingi tuwapeni Saport kwenye show ya jumamosi pale uwanjani leaders Club pia kwenye Kazi zao#Sio kuzomea haipendezi kabisa wala Sio Upendo tulionao watanzania #wote wanafanya Kazi nzuri kila mmoja ana mashabiki wake kelele za nini waacheni wafanye Kazi nzuri ili walitangaze taifa letu la #Tanzania nje ya tanzania uko kwenye upinzani Sio nyumbani? NAWATAKIA show NJEMA jumamoc iwe naamani mashabiki wote wa #KIBAna #dai’— @h_baba123

    Umeisikiliza single mpya ya staa wa kike wa filamu aliyomshirikisha A.T ? iko hapa



    .
    .
    Msanii wa kike wa filamu, Flora Mvungi time hii ameingia  pia kwenye tasnia ya Bongo Fleva ambapo leo ameachia single yake mpya iitwayo Mkazurure aliyomshirikisha A.T na kutayarishwa na producer Fraga kutoka Uprise Music.
    Isikilize hapa mtu wa nguvu kisha usisahau kuniandikia ya moyoni ili Flora Mvungi na A.T wakipita hapa wasome kutoka kwa watu wao wa nguvu..

    Nimerekodi Hekaheka ya leo Jan 20, inahusu msichana wa kazi aliyelalamika kunyanyaswa



    Hands
    Kama ulipitwa na  Hekaheka ya leo January 20 inatokea Dar, msichana mmoja aliyekuwa akifanya kazi za ndani alifika ofisi za Clouds FM akilalamikia kuteswa na bosi wake na kumtishia kumchoma kisu, alipoomba nauli ili arudi kwao bosi wake alikataa.
    Msichana huyo alitoroka na kuanza kuomba msaada ili aweze kupata shilingi elfu 60 kama nauli ya kurudi kwao.
    Bosi wake alipofuatwa alikiri kuwa msichana huyo alikuwa mfanyakazi wake, ameishi naye kwa muda mfupi  lakini alisitisha mkataba naye kutokana na binti huyo kuwa na ujauzito aliokuja nao kutoka Kigoma na ishu hiyo ilishafika hadi kituo cha Polisi.
    Bonyeza play kuisikiliza Hekaheka hiyo hapa.