Thursday, September 17, 2015

Mapenzi yake kwa Manchester City yamemfanya shabiki huyu wa Kihindi kuamua hivi..

By
on
Mpira wa miguu ni mchezo ulioteka hisia za watu wengi katika soka hususani wanaume, imekuwa ni kitu cha kawaida kuona mtu akijichora rangi mwilini mwake kama ishara ya kushangilia timu yake. Hili linaweza kuwa geni kwa ukanda wa Afrika Mashariki lakini Ulaya imezidi kushika kasi.
Suraj-Nandurkar
Shabiki wa klabu ya Manchester City Suraj Nandurkar ameingia kwenye headlines ya vyombo vya habari baada ya kuamua kuchora tattoo ya majina ya wachezaji waManchester City anaowapenda Suraj Nandurkar. Licha ya kukosea spelling majina ya Aleksandar Kolarov na Fernandinho, shabiki huyo anakiri kugundua kosa baada ya kumaliza kuchora.
Suraj-Nandurkar (1)
Suraj Nandurkar ambaye ana umri wa miaka 28 alianza kuipenda klabu ya Manchester City mwaka 2012 baada ya Sergio Aguero kufunga goli lililomvutia katika mechi dhidi yaQPRSuraj Nandurkar anafanya kazi na kuishi kwao Mumbai India.

Monday, September 14, 2015

MICHEZO

Hiki ndicho kilichowakuta Espanyol walipocheza na Real Madrid leo

By
Alpha Msigwa 
on
Ligi kuu ya Uhispania imeendelea leo baada ya mapumziko ya kupisha mechi za kimataifa kumalizika, Real Madrid walisafiri mpaka jijini Barcelona kwenda kucheza na Espanyol.
 
Mchezo uliopigwa katika dimba la Cornella El Plat umeshuhudia mwanasoka anayeshikilia taji la uchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo akifunga magoli 5 katika mchezo uliomalizika kwa Real Madrid kushinda 6-0.
 
Ilimchukua Cristiano Ronaldo dakika 20 tu kufunga hat trick katika dakika ya 7, 17 na 20, kabla ya Karim Benzema hajafinga goli la 4 katika dakika ya 28 na hivyo kupelekea Madrid kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa 4-0.
 
Kipindi cha Ronaldo akaongeza magoli mawili katika dakika ya 60 na 80 ya mchezo huo na hivyo kukamilisha ushindi wa 6-0

Baada ya kushinda pambano la 49, Floyd Mayweather anaachana na mchezo wa Ngumi??

By
Alpha Msigwa 
on
Bondia Floyd Mayweather ni jamaa mwenye rekodi nzuri ambayo ameijenga kwa kipindi chote cha miaka yote 19 aliyoitumia kwenye mchezo wa ngumi..Usiku wa kuamkia leo September 13 2015 kaiendeleza rekodi hiyo kwa kujiandikia ushindi mzuri baada ya kumpiga Bondia Andre Berto… Baada ya hapo kuna kinachofuatia??
Berto II
Stori ni nyingi kuhusu pambano lake na Manny Pacquiao kurudiwa, kuna stori kuhusu jamaa kuachana na mchezo wa Ngumi >>> ‘Nimekamilisha kila kitu, nimefanya kila kitu kwenye mchezo wangu… Umri wangu unakaribia miaka 40, hakuna nilichobakiza kwenye Ulimwengu wa Ngumi, nahitaji kutumia muda mwingi zaidi na familia yangu‘>> Hii ni moja ya nukuu ya alichokisema Floyd Mayweather baada ya pambano lake na Berto kuisha.
Baba yake Floyd anasema jamaa alilalamika sana maumivu ya mkono wakati akiendelea na pambano na Andre Berto, lakini hakuona kama ni tatizo kwa vile anaelekea kustaafu… Mayweather amemshinda Berto na kuandika headlines za ushindi wa 49 tangu alivyoanza mchezo wa Ngumi mwaka 1996.
Berto

Sunday, September 13, 2015

Pichaz za Birthday Party ya Ommy Dimpoz wakiwemo na mastaa mbalimbali

By
Alpha Msigwa
on
.
.
Sherehe za birthday nazo zina uzito wake, Unaambiwa msanii Omary Nyembo aka Ommy Dimpoz ambaye usiku wa Sept 13,2015 alishea siku yake ya kuzaliwa na watu mbalimbali wakiwemo mastaa wengi kutoka kwenye tasnia ya Bongo Fleva, kiukweli ilipendeza sanae.
Unaweza kucheki pichaz ambazo mtu wako wa nguvu nimekusogezea uzicheki na usipitwe pia.
.
.
.
.
.
.
.
Pichani:Mwanasheria Alberto Msando akiwa na mwigizaji Elizabeth Michael
.

Monday, September 7, 2015

Diamond Platnumz ametaja tarehe atakayoonekana sura mtoto wake (Tiffah)

Kama umekua ukifuatilia akaunti za Diamond Platnumz na mpenzi wake Zari tangu mtoto wao Tiffah azaliwe utakua umekutana na picha nusu ambayo anaonekana mtoto wao huyo na sehemu kubwa hua ni kuanzia kwenye kidevu kushuka chini.
tifHii imekua ni style nyingine ya mastaa wetu kadhaa kuchukua mfumo huu wa kutowapost au kuwaonyesha watoto wao hadi umri fulani ufike,Diamond Platnumz leo ametaja siku ambayo mtoto wao huyo ataonekana sura kwa wale ambao bado hawajapata nafasi ya kumuona.
                              By
                                   Prince Alpha.

Thursday, September 3, 2015

Hii ndio miji ya Africa inayokadiriwa kuja kuwa na mamilionea wengi kufikia 2020

Dunia inabadilika sana siku hizi mtu wangu, watu na wawekezaji wengi sana wanaitupia jicho Africa wakiamini hii ndio sehemu pekee iliyobaki yenye uwezo wa kuikomboa dunia ya kesho.
dsm
Dar Es Salaam Tanzania.
Nimekutana na stori moja kwenye mtandao inayosema kufikia mwaka 2020 Africa itakuwa ni miongoni mwa sehemu zitakazokuwa na ongezeko kubwa la Mamilionea wa Kiafrica, hii ni kutokana na utafiti uliofanyika na kuonyesha kama ukuaji wa uchumi na shughuli za kibiashara zikiendelea kukua kutakuwa hakuna haja wa Mamilionea wa Africa kuwekeza pesa zao sehemu nyingine.
JOBURG
Johannesburg South Africa.
Kati ya miji iliyotajwa kuwa na vigezo hivi ni mji wa Lagos wa Nigeria, Accra wa Ghana, Johannesburg wa South Africa na Dar es salaam wa Tanzania.
Kufikia mwaka 2012 Dar Es Salaam ilikuwa na idadi ya mamilionea 1,900 na makadirio yanaonyesha kutokana na ukuaji wa uchumi wetu wa Tanzania kufikia mwaka 2020 jiji la Dar es salaam litakuwa na idadi ya mamilionea wasiopungua 3,000!
Lagos Nigeria
Lagos Nigeria
Licha ya miji hii 4 kuwa yenye vigezo vikubwa zaidi nchi zingine za Africa zenye mamilionea wengi ni; mji wa Cairo uliopo Egypt, Cape Town uliopo South Africa, Kano ulipo Nigeria na Marrakesh uliopo Morroco.
CAIRO
Cairo Egypt.
cape town SA
Cape Town South Africa.
marrakesh morroco
Marrakesh Morroco.

Historia ya maisha ya Didier Drogba sasa kupatikana kwenye kitabu…

Drogba ni mmoja wa mastaa wakubwa Afrika na hata soka la Ulaya, Novemba mwaka huu anatarajia kuzindua kitabu kitakachozungumzia maisha yake kwa ujumla.
DDD
Akiwa na miaka yake 37 mshambuliaji huyo ameahidi kutoa kitabu hicho ambacho kitazungumzia pia na maisha yake akiwa Ufaransa, umuhimu wa elimu, jinsi ya kutafuta mafanikio katika maisha.

Itazme na hii mpya kutoka kwa Taylor Swift; ‘Wildest Dreams’ – (Video).

Baada ya kufanya show kali ya ufunguzi kwenye tuzo za MTV VMA’s 2015, Taylor Swift hajaona sababu ya kuishia hapo, Taylor karudi na hii mpya mtu wangu inaitwa ‘Wildest Dreams’, wimbo huu unapatikana kwenye Album yake mpya ‘1989’.
wild
Kama video ya wimbo huu bado haijakufikia karibu utizame hapa chini.