Wednesday, March 26, 2014

Hii ndio historia aliyoiandika Pep Guardiola baada ya Bayern Munich kutwaa ubingwaBAYERN-0111_600_396_100Kocha Pep Guardiola jana usiku aliandika historia akiwa na klabu ya Bayern Munich baada ya kuiongoza klabu hiyo kutwaa ubingwa wa Bundesliga      10154423_10152099255323598_1013413957_n-1Historia aliyoandika Guardiola ni kuiongoza FC Bayern München kutwaa ubingwa wa 23 wa Bundesliga baada ya michezo 27 tu huku wakiwa hawajapoteza mchezo hata mmoja kwenye ligi – huu ndio ubingwa wa haraka zaidi katika historia ya Bundesliga.

Ubingwa huu ni wa tatu kwa Pep Guardiola katika msimu wake wa kwanza, alishinda UEFA Super Cup mwaka jana mwezi August, kisha wakashinda ubingwa wa klabu bingwa ya dunia December mwaka jana.

No comments:

Post a Comment