Tuesday, November 26, 2013

WANAIGERIA WAMWEKA KITI MOTO DIAMOND KWA KUVAA VIBAYA KWENYE ARUSI YA PETER WA P-SQUARE MA2KIO NA PRINCE ALPHA.So Diamond Platnumz jana alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa waliohudhuria harusi ya kimila ya Peter Okoye wa kundi la P-Square na mchumba wake, Lola Omotayo iliyofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Kwenye harusi hiyo, Diamond alipata nafasi ya si tu kushuhudia Peter na Lola wakisema ‘Yes I do’ bali pia aliweza kuchill na cream ya mastaa wa Afrika wakiwemo Iyanya na mchezaji wa timu ya Tottenham Hotspur na timu ya taifa ya Togo, Emmanuel Adebayor.

Alipata pia fursa ya kuwaonesha Adebayor na Iyanya style yake ya kucheza ya Ngololo

Hata hivyo, kitu kimoja hakikwenda sawa. Ni nguo aliyokuwa ameivaa, ambayo iligeuka gumzo kwa mashabiki wengi wa muziki nchini Nigeria waliosema kachemka. BY ALPHA MSIGWA 0764849514

No comments:

Post a Comment