Saturday, December 14, 2013

Watu 41 akiwemo waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa wanusurika kifo baada ya ndege waliyopanda kupasuka matairi
Abiria 37 na wafanyakazi 4 wa ndege ya Precision Air wamenusurika kifo baada ya ndege waliyokuwa wamepanda kupasuka matairi wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa Arusha leo majira ya mchana.

Waziri mkuu mstaafu ambaye ni mbunge wa Monduli, Edward Lowassa alikuwa miongoni mwa abiria wa ndege hiyo waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Arusha.  
Shirika la ndege la Precision Air limetoa tamko rasmi kwa umma, ambapo limeeleza kuwa watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo wako salama.
Tamko la Precision Air baada ya ndege yao kupasuka matairi.

No comments:

Post a Comment