Saturday, December 21, 2013

Diamond Platnumz akimmwagia manoti Halima Kimwana.

Stori: Hamida Hassan na Musa Mateja
KUFURU ya kufunga mwaka! Dogo anayejua kuzitumia vyema fursa muhimu, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ amefanya yake kwa mara nyingine, safari hii amefanya pati iliyojaa ufuska, Ijumaa linaibumburua.
Burudani zikitolewa na Kundi la Kibao Kata.
Msanii huyo kwa ‘kolabo’ ya swahiba wake mkuu ndani ya anga la muziki Bongo, Omari Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ alifanya tukio hilo lililoacha watu midomo wazi mwanzoni mwa wiki hii ndani ya Ukumbi wa Business Park uliopo Kijitonyama, Dar.
Pati hiyo ilikuwa ya kumpongeza mtu wake wa karibu katika Wasafi Classic Baby (WCB), Halima Haroun ‘Halima Kimwana’.
Halima Kimwana akionyesha baadhi ya manoti aliyotunzwa.
FUNUNU ZA PATI
Ngoma za masikio ya ‘viranja’ wetu yalinasa fununu za kuwepo kwa kufuru hiyo mapema mwishoni mwa wiki iliyopita na kuanza kuandaa ‘patroo’ maalumu ili kunasa matukio muhimu.
SIKIA FUNUNU ZENYEWE
Akizungumza na waandishi wetu kwa usiri na sauti ya ‘kimbeya’, mmoja wa rafiki wa Diamond (jina kapuni) aliweka wazi kwamba Diamond alipania kumfanyia Halima pati hiyo ikiwa ni moja ya matukio yatakayoendelea
Mmoja wa wasanii wa Kundi la Kibao Kata akifanya vitu vyake.
“Diamond amepania kufanya makubwa kwenye sherehe hiyo ya kuzaliwa ya Halima ikiwa ni moja ya matukio yake muhimu yatakayokumbukwa. Itakuwa ni pati ya kufa mtu,” alisema ‘kikulacho’ huyo.
MAANDALIZI
Duru za habari zilizidi kudai kuwa, maandalizi ya sherehe hiyo yaliingiliwa kati na Diamond na kumzuia Halima asitumie fedha zake na kwamba kila kitu na gharama zote za juu zitakuwa juu yake.
Steve Nyerere naye akitoa 'misimbazi' kwa Halima.
SIKIA HII
Katika moja ya maandalizi ya sherehe hiyo, walialikwa wacheza shoo maalumu ‘Kibao Kata’ wakiwemo wake za watu ambao siku hiyo walifanya ‘usodoma’ uliomfanya hata shetani mwenyewe afumbe macho kwa aibu.
SIKU YA SIKU
Hatimaye siku ya sherehe hiyo iliwadia Jumatatu ya wiki hii, mastaa muhimu wa mrembo huyo wakaalikwa. Ngoma ya Kibao Kata na muziki wakalamba 500,000, ikawa ni mwendo wa kumwaga lazi kwa kwenda mbele.
Diamond na Ommy Dimpoz (kulia) wakipata msosi katika 'bethidei' hiyo. Kushoto nyuma ni msanii Shetta.
Katika sherehe hiyo ambayo Halima Kimwana alitimiza miaka kadhaa tangu aanze kuvuta hewa ya oksijeni, muziki wa ladha mbalimbali ulitawala huku nyimbo za ‘kaka mdogo‘ huyo zikichosha ngoma za masikio ya wahudhuriaji.
‘MISIMBAZI’ YATAWALA
Ili neno historia litimie, Diamond alifungua ukurasa wa kumwagia Halima ‘mvua’ ya noti nyingi za shilingi elfu kumikumi zilizokadiriwa kuwa Sh. milioni moja na ushee.
kukumbukwa kwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment